Papa Sixtus I (au Xystus) alikuwa Papa kuanzia takriban 117/119 hadi kifo chake takriban 126/128[1][2]. Alitokea Roma, Italia na jina la baba yake lilikuwa Pastor[3].
Alimfuata Papa Alexander I akafuatwa na Papa Telesphorus[4].
Alishughulikia liturujia ya Kanisa la Roma [5] bila kulazimisha majimbo mengine hata kuhusu suala la adhimisho la Pasaka ya Kikristo lililoanza kujitokeza.
Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu mfiadini na kutajwa katika Kanuni ya Kirumi.
Sikukuu yake ni tarehe 3 Aprili[6].