Metali adimu
Metali adimu ni metali zenye tabia ya kutomenyuka kwa urahisi. Haziguswi na maji au oksijeni ya hewa, tofauti na metali nyingi. Mara nyingi hutazamwa kuwa metali za thamani kwa sababu zinadumu na kuwa haba. Mifano yake ni dhahabu (auri), fedha (ajenti), shaba (kupri), tantali, platini, paladi na rhodi. Kuhusu shaba maoni hutofautiana kama inahesabiwa humo. Elementi sintetiki za Bohri, Hassi, Meitneri, Darmstati na Roentgeni zatazamwa pia kama metali adimu hata kama hazina matumizi kutokana na maisha mafupi ya elementi hizo. Matumizi ya metali adimuMetali adimu, hasa dhahabu na fedha, zilitumiwa kwa mapambo ya thamani kwa watu. Katika tamaduni mbalimbali dhahabu ilikuwa metali ya mfalme au mwene. Zilifaa pia kwa biashara kwa sababu zilitafutwa na watu kote zikabebwa kwa urahisi na kudumu. Hivyo vipande vya metali hizo vilipimwa kufuatana na uzito vikatumiwa kwa biashara. Baadaye vipande vyenye uzito maalumu viligongwa mhuri na kuwa chanzo cha pesa. ![]()
|