WikiHowWikiHow ni wavuti inayonyesha jinsi ya kufanya mambo na maswali kwenye mada mbalimbali kupitia mtandao. Wavuti ilianzishwa mwaka 2005 na mjasiriamali wa mtandao Jack Herrick. Lengo lake ni kuunda kanzidata kubwa ya maudhui ya maelekezo, ikitumia mfano wa wiki kama maarifu huru ya ujenzi wa taarifa zake. Watumiai wanaweza kuongeza, kuunda, na kurekebisha maudhui. Ni shirika mseto, kampuni inayotengeneza faida inayosimamiwa kwa ajili ya dhamira ya kijamii. WikiHow inatumia toleo lililotofautishwa la programu ya MediaWiki ambalo ni huru na ya chanzo huru; mabadiliko haya yaliyofanywa na wikiHow yalipatikana kwa umma kupitia tovuti ya kupakua ya kujihudumia kutoka mwaka 2010 hadi mwishoni mwa 2020. Wakati wikiHow ilipoamua kusitisha tovuti ya kujihudumia, ikinukuu "mashambulizi ya DoS" yasiyoeleweka, pamoja na kusema kuwa kuchapisha msimbo wa chanzo si "sehemu ya dhamira yetu kuu." [1][2][3] Maudhui ya maandishi ya tovuti yanatolewa chini ya leseni ya Creative Commons NonCommercial. Mnamo Februari 2005, wikiHow ilikuwa na zaidi ya wageni milioni 35.5 wa kipekee. Kufikia Desemba 2021, wikiHow ilikuwa na zaidi ya makala 235,000 za jinsi ya kufanya mambo na watumiaji waliosajiliwa zaidi ya milioni 2.5. Marejeo
|