Share to: share facebook share twitter share wa share telegram print page

Ada Udechukwu

Ada Udechukwu (alizaliwa Enugu, 1960) ni msanii na mshairi kutoka Nigeria anayehusishwa na kundi la Nsukka.[1]

Wasifu

Udechukwu alizaliwa katika mji wa Enugu, uliopo kusini mashariki mwa Nigeria. Yeye ni binti wa baba wa kabila la Waigbo na mama Mmarekani

Wakati sehemu ya kusini mashariki ya Nigeria ilipojaribu kujitenga na Nigeria na kuunda jamhuri ya Biafra, hali hii ilisababisha vita ya wenyewe kwa wenyewe iliyojulikana kama vita ya Biafra ya mwaka 1967-70. Kutokana na vita yeye pamoja na ndugu zake walikimbilia Michigan, Marekani pamoja na mama yao huku baba yao alibaki Nigeria. Walibaki Michigan mpaka mwaka 1971, mwaka baada ya vita ya Biafra kuisha.[2]

Alisoma chini ya mwandishi Chinua Achebe, akapata shahada ya kwanza ya lugha ya Kiingereza na fasihi katika Chuo Kikuu cha Nigeria, Nsukka. Alianza kuchora kwenye vitambaa, michoro kwenye mavazi kwa kutumia mtindo wa mstari wa kujizuia. Mwaka 1988, alianza kuchora kwenye karatasi akitumia wino na rangi za maji. Michoro hiyo ni ya binafsi zaidi kuliko kazi zake nyingine, ikiakisi juhudi zake za kusawazisha maisha ya kuwa mwanamke na msanii. Kazi zake piahhuchunguza changamoto za utambulisho wa kitamaduni na wa tamaduni mseto ndani na nje ya Afrika. Kazi zake ni mkusanyo wa The Newark Museum of Art.[3][4] Udechukwu ni miongoni wasanii wachche wanawake waliohusishwa na kundi la Nsukka.[5]

Mnamo mwaka 1997,wakati wa kilele cha utawala wa kijeshi nchini Nigeria, mumewe Obiora Udechukwu alikubali nasafi ya kufundisha katika chuo kikuu cha St Lawrence, kilichopo katika sehemu ya Kaskazini ya jimbo la New York,Marekani. Binti yao, Ijeanuli pamoja na kijana wao, Nwora wanandoa hao waliondoka Nigeria kuelekea Marekani amabako wamekuwa wakiishi tangu wakati huo.

Kama mwandishi, Ada Udechukwu ni mshairi kwa kiasi kikubwa. Pia anajilikana ama mwandishi wa hadithi fupi. Kitabu chake cha Mashiri na Michioro, Woman,Me,[6] kilichapishwa na Boomerang Press mwaka 1993.Hadithi yake fupi "Night Bus" ilichapishwa katika loleo maalumu la hadithi za kubuni la jarida The Atlantic(Agosti 2006). Pia alichapisha kitabu cha watoto kinachoitwa Herero, mnamo mwaka 1995.[7]

Marejeo

  1. "The Poetics of Line". africa.si.edu. Iliwekwa mnamo 2020-05-28.
  2. "Out of the Darkness". The Atlantic. 11 Julai 2006.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. "Search Our Collection | Newark Museum". www.newarkmuseumart.org. Iliwekwa mnamo 2020-03-07.
  4. Cotter (15 Agosti 2013). "Nigeria in the Middle of Newark". The New York Times.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  5. "The Poetics of Line". africa.si.edu. Iliwekwa mnamo 2020-03-07.
  6. Udechukwu, Ada Obi, 1960- (1993). Woman, me. Bayreuth, Germany: Boomerang Press. ISBN 3-9802212-7-X. OCLC 28832296.{{cite book}}: CS1 maint: multiple names: authors list (link) CS1 maint: numeric names: authors list (link)
  7. Udechukwu, Ada (1995). Herero. New York: Rosen. ISBN 9780823920037.
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ada Udechukwu kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Prefix: a b c d e f g h i j k l m n o p q r s t u v w x y z 0 1 2 3 4 5 6 7 8 9

Portal di Ensiklopedia Dunia

Kembali kehalaman sebelumnya