Share to: share facebook share twitter share wa share telegram print page

Abu Bakr al-Siddiq

Abu Bakr al-Siddiq (pia alijulikana kama Edward Doulan) alikuwa msomi wa Kiislamu kutoka mji wa Timbuktu (Mali). Akiwa kijana wa miaka ishirini na kitu alitekwa na kufanywa mtumwa katika mji wa Bouna (wilaya)|Bouna (ulio katika eneo la leo la Kodivaa). Aliandika wasifu wake binafsi, yaani simulizi ya maisha yake akiwa mtumwa, kwa lugha ya Kiarabu. Nakala mbili (moja ikiwa Jamaika na nyingine karibu na London) zilitafsiriwa kwa Kiingereza na kuchapishwa mwaka 1834.

Abu Bakr al-Siddiq alikuwa mtoto wa mfanyabiashara maarufu na msafiri, ambaye alienda Bouna kutafuta dhahabu. Abu Bakr alielekezwa katika masomo ya Kiislamu mjini Jenne baada ya kifo cha baba yake huko Bouna alipokuwa safarini. Baadaye alisafiri kwenda kuzuru kaburi la baba yake akiwa na mwalimu wake. Walipokuwa wakiishi huko, vita vilizuka; Adrinka, Sultani wa Bondoukou, alimuua Sultani wa Banda Besar na kupanua vita hadi Bouna, ambapo jeshi lake liliteka mji huo. Kwenye machafuko hayo, Abu Bakr alikamatwa na kufanywa mtumwa. Alipewa mzigo mkubwa kubeba hadi pwani ya Atlantiki, ambako aliuzwa kwa watu wa Kikristo, na baada ya safari ya miezi mitatu baharini, walifika Jamaika. Barua mbili zilizoandikwa mwishoni mwa simulizi yake zinaeleza kuwa alikuja kuachiwa huru na mmiliki wake, Alexander Anderson, na hapo ndipo alipatiwa jina lake la Kiingereza kama Edward Doulan.[1][2]

Marejeo

  1. Kalu, Anthonia C., mhr. (2007). "The African Travels of Abu Bakr al-Siddiq". The Rienner Anthology of African Literature. Boulder: Lynn Rienner. ku. 200–205. ISBN 9781626375833.
  2. Al-Ahari, Muhammad A., mhr. (2006). "'Abu Bekr Sheriff of Timbuktoo; Written in Jamaica 1834". Five Classic Muslim Slave Narratives. American Islamic Heritage Series. Chicago: Magribine Press. ku. 201–207. ISBN 9781463593278.
Prefix: a b c d e f g h i j k l m n o p q r s t u v w x y z 0 1 2 3 4 5 6 7 8 9

Portal di Ensiklopedia Dunia

Kembali kehalaman sebelumnya